Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

ISO 9001:2015 Imethibitishwa Kutoa Huduma za Hali ya Hewa kwenye Usafiri wa Anga

Monthly Forecast

MWELEKEO WA HALI YA HEWA MWEZI JULAI 2026

Dondoo za tathmini ya Juni, 2026 na mwelekeo wa Julai, 2026:

Taarifa hii inatoa muhtasari wa mifumo ya hali ya hewa pamoja na mwenendo wa hali ya hewa kwa mwezi Juni, 2026 na kutoa mwelekeo wa hali ya hewa hususan hali ya joto kwa mwezi Julai, 2026 nchini.

  • Katika kipindi cha mwezi Juni, 2026 baadhi ya maeneo nchini yaliendelea kupata vipindi vya baridi ya wastani hadi baridi kali, hususan nyakati za usiku na asubuhi.
  • Vipindi vya upepo mkali vilijitokeza katika baadhi ya maeneo katika kipindi cha mwezi Juni 2026, hususan ukanda wa pwani na maziwa makuu. Aidha, vipindi vya mvua vilijitokeza katika maeneo machache ya mwambao wa pwani, ukanda wa ziwa Victoria na maeneo ya miinuko ya nyanda za juu kaskazini mashariki na kusini magharibi.
  • Katika kipindi cha mwezi Juali 2026 hali ya joto la chini inatarajiwa  kuendelea kupungua katika maeneo mengi ya nchi. Aidha, vipindi vya mvua vinatarajiwa katika maeneo machache, hususan mwambao wa pwani, ukanda wa Ziwa Victoria na maeneo yenye miinuko ya nyanda za juu kaskazini mashariki.Pia, vipindi vya upepo mkali vinatarajiwa kujitokeza katika baadhi ya maeneo.

Kwa taarifa zaidi tafadhali pakua hapa