Taarifa za Utabiri
Mvua na ngurumo zinatarajiwa kuendelea katika ukanda wa ziwa Victoria
Kwa taarifa zaidi tafadhali pakua..........
MWELEKEO WA MVUA KWA TAREHE 11-20 SEPTEMBA, 2025
Kanda ya ziwa Viktoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Mwanza, Simiyu na Mara): Vipindi vya mvua zinazoambatana na ngurumo za radi vinatarajiwa katika maeneo machache.
Nyanda za juu kaskazini-mashariki (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro): Hali ya ukavu kwa ujumla inatarajiwa.
Pwani ya kaskazini (Mikoa ya Tanga, Maeneo ya kaskazini mwa Morogoro, Pwani na Dar es Salaampamoja na visiwa vya Unguja na Pemba): Vipindi vya mvua vinatarajiwa katika maeneo machache hasa katika kipindi cha pili cha dekad.
Magharibi mwa nchi (Mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora): Hali ya ukavu inatarajiwa.
Kanda ya kati (Mikoa ya Dodoma na Singida): Hali ya ukavu inatarajiwa.
Nyanda za juu Kusini-magharibi (Mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa): Hali ya ukavu inatarajiwa.
Pwani ya kusini (Mikoa ya Mtwara na Lindi): Vipindi vya mvua nyepesi vinatarajiwa katika maeneo machache hasa katika kipindi cha pili cha dekad.
Kanda ya kusini (Mkoa wa Ruvuma na Maeneo ya kusini mwa Morogoro): Hali ya ukavu inatarajiwa.
Imetolewa na:
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Kwamaelezo zaidi tafadhali pakua...
Dondoo za tathmini ya Agosti, 2025 na mwelekeo wa Septemba, 2025:
Taarifa hii inatoa muhtasari wa mifumo ya hali ya hewa pamoja na mwenendo wa hali ya hewa kwa mwezi Agosti, 2025 na kutoa mwelekeo wa hali ya hewa hususan hali ya joto kwa mwezi Septemba, 2025 nchini.
- Katika kipindi cha mwezi Agosti, 2025 hali ya baridi ilijitokeza katika baadhi ya maeneo nchini, hususani nyakati za usiku na asubuhi. Hali ya baridi zaidi ilijitokeza katika maeneo ya nyanda za juu kusini magharibi.
- Vipindi vifupi vya mvua zilizoambatana na radi vilijitokeza katika maeneo machache ya Ziwa Victoria. Hata hivyo, ukanda wa pwani pamoja na nyanda za juu kaskazini mashariki vilipata vipindi vya mvua nyepesi katika maeneo machache. Aidha, vipindi vya upepo mkali unaofikia kasi ya kilometa 40 kwa saa vilijitokeza katika baadhi ya maeneo nchini.
- Kwa mwezi Septemba 2025, hali ya baridi inatarajiwa kuendelea katika baadhi ya maeneo nchini hususani katika maeneo ya nyanda za juu kusini magharibi ikiambatana na hali ya ukavu kwa ujumla. Aidha, vipindi vichache vya mvua vinatarajiwa katika maeneo ya mwambao wa pwani, ukanda wa Ziwa Victoria, na maeneo ya miinuko ya nyanda za juu kaskazini mashariki.
Kwa maelezo zaidi, tafadhali pakua
Dondoo muhimu za msimu wa mvua za Vuli kipindi cha Oktoba – Desemba, 2025
Taarifa hii inatoa uchambuzi wa mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa na mwelekeo wa msimu wa mvua za Vuli kipindi cha Oktoba - Disemba 2025, ushauri na tahadhari kwa wadau wa Sekta mbalimbali kama vile Kilimo na Usalama wa chakula, Mifugo na Uvuvi, Utalii na Wanyamapori, Usafiri na Usafirishaji (nchi kavu, kwenye maji na angani), Mamlaka za miji, Sekta binafsi, Vyombo vya habari, Nishati, Maji na Madini, Afya pamoja na Menejimenti za maafa. Utabiri huu ni mahsusi kwa maeneo (Nyanda za juu kaskazini mashariki, Pwani ya kaskazini, Ukanda wa Ziwa Viktoria pamoja na kaskazini mwa mkoa wa Kigoma) yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka. Kwa muhtasari, mwelekeo huo na athari zake unaonesha kuwa:
a) Mvua za Vuli, 2025
i. Mvua zinatarajiwa kuwa za Wastani hadi Chini ya Wastani katika maeneo mengi na kutawaliwa na vipindi virefu vya ukavu na mtawanyiko wa mvua usioridhisha hususan katika maeneo ya pwani ya kaskazini na nyanda za juu kaskazini mashariki.
ii. Mvua zinatarajiwa kuanza wiki ya kwanza na ya pili ya mwezi Oktoba, 2025 katika maeneo ya mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Mara na kaskazini mwa mkoa wa Kigoma; na kusambaa katika maeneo ya pwani ya kaskazini na nyanda za juu kaskazini mashariki wiki ya kwanza na ya pili ya mwezi Novemba 2025. Mvua zinatarajiwa kuisha mwezi Januari, 2026.
iii. Mvua za Vuli zinatarajiwa kuongezeka kidogo mwezi Desemba, 2025.
iv. Vipindi vya joto kali kuliko kawaida vinatarajiwa katika msimu huu wa Vuli.
b) Athari zinazotarajiwa
i. Upungufu wa unyevunyevu katika udongo unatarajiwa kujitokeza katika maeneo mengi na hivyo kuathiri shughuli za kilimo.
ii. Kunatarajiwa kupungua kwa kina cha maji katika mito, mabwawa na hifadhi ya maji ardhini.
iii. Kunatarajiwa kujitokeza kwa magonjwa ya mlipuko, kutokana na upungufu wa maji safi na salama.
Kwa maelezo zaidi rafadhali pakua.
Dar es Salaam |
|||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|
Tarehe | Hali ya Mchana | Kiwango cha Juu cha Joto | Kiwango cha Chini cha Joto | Mawio ya Jua | Machweo ya Jua | ||
17/09/2025 |
![]() Mvua |
28°C | 24°C | 06:19 | 18:20 | ||
17/09/2025 |
![]() Mvua |
28°C | 24°C | 06:19 | 18:20 | ||
18/09/2025 |
![]() Mvua |
28°C | 24°C | 06:19 | 18:20 | ||
17/09/2025 |
![]() Mvua |
31°C | 20°C | 06:19 | 18:20 | ||
18/09/2025 |
![]() Mvua |
30°C | 20°C | 06:19 | 18:20 |