Taarifa za Utabiri
ANGALIZO la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita 2, limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa Pwani ya bahari ya Hindi (mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba).
MWELEKEO WA MVUA KWA TAREHE 11- 20 MEI, 2024
Kanda ya ziwa Viktoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Mwanza, Simiyu na Mara): Mvua na ngurumo za radi vinatarajiwa katika maeneo machache.
Nyanda za juu kaskazini-mashariki (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro): Vipindi vya mvua nyepesi vinatarajiwa katika maeneo machache.
Pwani ya kaskazini (Mikoa ya Tanga, Maeneo ya kaskazini mwa Morogoro, Pwani na Dar es Salaampamoja na visiwa vya Unguja na Pemba): Vipindi vya mvua vinatarajiwa katika maeneo machache.
Magharibi mwa nchi (Mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora): Mvuana ngurumo za radi vinatarajiwa katika maeneo machache.
Kanda ya kati (Mikoa ya Dodoma na Singida): Vipindi vya ukavu kwa ujumla vinatarajiwa.
Nyanda za juu Kusini-magharibi (Mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa): Mvua zinatarajiwa katika maeneo machache hasa yale yenye miinuko.
Pwani ya kusini (Mikoa ya Mtwara na Lindi): Mvua nyepesi zinatarajiwa katika maeneo machache.
Kanda ya kusini (Mkoa wa Ruvuma na Maeneo ya kusini mwa Morogoro): Vipindi vya ukavu kwa ujumla vinatarajiwa.
Imetolewa na;
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Dondoo za tathmini ya Aprili, 2024 na mwelekeo wa Mei, 2024:
Taarifa hii inatoa muhtasari wa mifumo ya hali ya hewa pamoja na mwenendo wa hali ya hewa kwa mwezi Aprili, 2024 pamoja na mwelekeo wa hali ya hewa kwa mwezi Mei, 2024 nchini.
- Katika kipindi cha mwezi Aprili, 2024 vipindi vya mvua vilijitokeza katika baadhi ya maeneo nchini mengi pamoja na vipindi vya mvua kubwa katika baadhi ya maeneo na kusababisha mafuriko, uharibifu wa mali, miundombinu na upotevu wa maisha.
- Katika kipindi cha mwezi Mei 2024, mvua zinatarajiwa kuendelea katika baadhi ya maeneo hususan yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka. Aidha, ongezeko la mvua linatarajiwa katika maeneo machache.
- Joto la kawaida hadi chini kidogo ya kawaida linatarajiwa katika maeneo mengi ya nchi kwa kipindi cha mwezi Mei, 2024.
Kwa maelezo zaidi, tafadhali pakua
Dondoo muhimu za msimu wa mvua za Masika; Machi - Mei 2024 Taarifa hii inatoa uchambuzi wa mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa na mwelekeo wa msimu wa mvua za Masika katika kipindi cha Machi – Mei, 2024, ushauri kwa wadau wa sekta na mamlaka mbalimbali kama vile Kilimo na Usalama wa Chakula, Mifugo na Uvuvi, Utalii na Wanyamapori, Uchukuzi, Mamlaka za miji, Nishati, Maji na Madini, Afya pamoja na Menejimenti za Maafa. Baadhi ya mambo muhimu katika taarifa hii ni: - i. Mvua za Wastani hadi Juu ya Wastani kwa msimu wa Masika, 2024 zinatarajiwa katika maeneo mengi ya nchi yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka. ii. Ongezeko la mvua linatarajiwa katika kipindi cha mwezi Machi, 2024. iii. Mvua za Masika zinatarajiwa kuanza wiki ya nne ya mwezi Februari, 2024 katika maeneo mengi na zinatarajiwa kuisha katika wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Mei 2024 katika maeneo mengi. Athari zinazotarajiwa: i. Vipindi vya unyevu wa kuzidi kiasi pamoja na mafuriko vinaweza kujitokeza na kuathiri ukuaji wa mazao na miundombinu ya kilimo. ii. Kina cha maji katika mito na mabwawa kinatarajiwa kuongezeka. iii. Magonjwa ya mlipuko yanaweza kujitokeza kutokana na uchafuzi wa maji |
Dar es Salaam |
|||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|
Tarehe | Hali ya Mchana | Kiwango cha Juu cha Joto | Kiwango cha Chini cha Joto | Mawio ya Jua | Machweo ya Jua | ||
20/05/2024 |
Vipindi vya Jua |
33°C | 22°C | 06:26 | 18:12 | ||
21/05/2024 |
Vipindi vya Jua |
33°C | 23°C | 06:26 | 18:12 | ||
20/05/2024 |
Vipindi vya Jua |
32°C | 23°C | 06:26 | 18:12 | ||
21/05/2024 |
Mvua Nyepesi |
31°C | 23°C | 06:27 | 18:11 | ||
20/05/2024 |
Vipindi vya Jua |
32°C | 22°C | 06:26 | 18:12 |