Taarifa za Utabiri
Upepo wa Pwani: Unatarajiwa kuvuma kutoka Mashariki kwa kasi ya km 30 kwa saa kwa Pwani yote. Hali ya Bahari: Inatarajiwa kuwa na Mawimbi Makubwa Kiasi.
MWELEKEO WA MVUA KWA TAREHE 01-10 DESEMBA, 2025
Kanda ya ziwa Victoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Mwanza, Simiyu na Mara): Vipindi vya mvua zinazoambatana na ngurumo za radi vinatarajiwa katika maeneo machache hususan katika kipindi cha siku tano za mwisho.
Nyanda za juu kaskazini-mashariki (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro): Hali ya ukavu kwa ujumla inatarajiwa.
Pwani ya kaskazini (Mikoa ya Tanga, Maeneo ya kaskazini mwa Morogoro, Pwani na Dar es Salaampamoja na visiwa vya Unguja na Pemba): Vipindi vyamvua nyepesi vinatarajiwa katika maeneo machache hususan katika kipindi cha siku tano za mwisho.
Magharibi mwa nchi (Mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora): Mvua zinazoambatana na ngurumo za radi zinatarajiwa katika maeneo machache ya mikoa ya Kigoma na Katavi hususan katika kipindi cha siku tano za mwisho.
Kanda ya kati (Mikoa ya Dodoma na Singida): Hali ya ukavu kwa ujumla inatarajiwa.
Nyanda za juu Kusini-magharibi (Mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa): Vipindi vya mvua vinatarajiwa katika maeneo machache hususan katika kipindi cha siku tano za mwisho.
Pwani ya kusini (Mikoa ya Mtwara na Lindi): Vipindi vya mvua nyepesi vinatarajiwa katika maeneo machache hususan katika kipindi cha siku tano za mwisho.
Kanda ya kusini (Mkoa wa Ruvuma na Maeneo ya kusini mwa Morogoro):Vipindi vya mvua vinatarajiwa katika maeneo machache hususan katika kipindi cha siku tano za mwisho.
Imetolewa na:
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Kwa maelezo zaidi tafadhali pakua...
Dondoo za tathmini ya Novemba, 2025 na mwelekeo wa Desemba, 2025:
Taarifa hii inatoa muhtasari wa mifumo ya hali ya hewa pamoja na mwenendo wa hali ya hewa kwa mwezi Novemba, 2025 na kutoa mwelekeo wa hali ya hewa kwa mwezi Desemba, 2025 nchini.
i. Katika kipindi cha mwezi Novemba, 2025 vipindi vya mvua vilijitokeza katika maeneo machache nchini, hususan ukanda wa pwani, ukanda wa Ziwa Victoria na magharibi mwa nchi. Aidha, vipindi vichache vya mvua kubwa vilijitokeza.
ii. Katika kipindi cha mwezi Desemba 2025, mvua zinatarajiwa katika baadhi ya maeneo zikiwa na mtawanyiko usioridhisha. Aidha, vipindi vichache vya mvua kubwa vinatarajiwa katika maeneo machache.
iii. Hali ya joto inatarajiwa kuendelea katika maeneo yanayotarajiwa kuwa na upungufu wa mvua.
Kwa maelezo zaidi, tafadhali pakua...
Dondoo muhimu za mvua za Msimu (Novemba, 2025 – Aprili, 2026)
Taarifa hii inatoa uchambuzi wa mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa na mwelekeo wa mvua za Msimu kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka (kanda ya magharibi, kati, nyanda za juu kusini magharibi, kusini mwa nchi, ukanda wa pwani ya kusini pamoja na maeneo yaliyopo kusini mwa Mkoa wa Morogoro) katika kipindi cha miezi ya Novemba, 2025 hadi Aprili, 2026. Ushauri na tahadhari umetolewa kwa wadau wa sekta mbalimbali wanaotumia taarifa za hali ya hewa katika utekelezaji wa majukumu yao kama vile kilimo na usalama wa chakula, mifugo na uvuvi, maliasili, wanyamapori na utalii, nishati na maji, ujenzi, usafiri na usafirishaji (nchi kavu, kwenye maji na angani), mamlaka za miji, afya, sekta binafsi pamoja na menejimenti za maafa. Muhtasari wa mwelekeo wa mvua hizo na athari zake ni kama ifuatavyo:
a) Mwelekeo wa mvua za Msimu kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka:
(i) Mvua za Chini ya Wastani hadi Wastani zinatarajiwa katika mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi, Singida na Dodoma. Aidha, mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani zinatarajiwa katika mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya, Songwe, Rukwa, Ruvuma, Mtwara na Lindi pamoja na kusini mwa mkoa wa Morogoro. Msimu unatarajiwa kutawaliwa na vipindi virefu vya ukavu na mtawanyiko wa mvua usioridhisha katika maeneo mengi.
(ii) Mvua zinatarajiwa kuanza kati ya wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Oktoba, 2025 katika mikoa ya Tabora, Katavi na Kigoma; na kusambaa katika mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe pamoja na kusini mwa mkoa wa Morogoro kati ya wiki ya pili na ya tatu ya mwezi Novemba, 2025. Mvua hizi zinatarajiwa kuisha kati ya wiki ya nne ya mwezi Aprili na wiki ya kwanza ya mwezi Mei 2026 katika maeneo mengi.
(iii) Kipindi cha nusu ya pili ya msimu (Februari – Aprili, 2026) kinatarajiwa kuwa na ongezeko la mvua ikilinganishwa na nusu ya kwanza (Novemba, 2025 – Januari, 2026).
b) Athari na ushauri
(i) Mvua za Chini ya Wastani zinazotarajiwa katika maeneo mengi zinaweza zikasababisha upungufu wa unyevu wa udongo, jambo ambalo linaweza kuathiri ukuaji na maendeleo ya mazao na kupunguza mavuno hususani kwa mazao yanayategemea mvua.
(ii) Kupungua kwa kina cha maji kwenye mabwawa na mtiririko wa maji kwenye mito kunaweza kutokea, hali ambayo inaweza kupunguza upatikanaji wa maji kwa matumizi mbalimbali.
(iii) Upatikanaji wa maji na malisho kwa ajili ya mifugo unatarajiwa kuathirika.
Kwa maelezo zaidi rafadhali pakua.
Dar es Salaam |
|||||||
|---|---|---|---|---|---|---|---|
| Tarehe | Hali ya Mchana | Kiwango cha Juu cha Joto | Kiwango cha Chini cha Joto | Mawio ya Jua | Machweo ya Jua | ||
| 06/12/2025 |
Mvua Nyepesi |
33°C | 25°C | 05:59 | 18:27 | ||
| 06/12/2025 |
Mvua Nyepesi |
34°C | 25°C | 05:59 | 18:27 | ||
| 07/12/2025 |
Mvua Nyepesi |
34°C | 25°C | 05:59 | 18:27 | ||
| 06/12/2025 |
Mvua Nyepesi |
33°C | 24°C | 05:59 | 18:27 | ||
| 07/12/2025 |
Mvua Nyepesi |
34°C | 24°C | 05:59 | 18:27 | ||
