Machapisho

MATARAJIO YA HALI YA HEWA KWA TAREHE 21 - 31 JANUARI, 2024

Pakua

MWELEKEO WA MVUA KWA TAREHE 21-31 JANUARI, 2024

Kanda ya ziwa Viktoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Mwanza, Simiyu na Mara): Mvua na ngurumo za radi vinatarajiwa katika maeneo machache.

Nyanda za juu kaskazini-mashariki (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro): Vipindi vya mvua vinatarajiwa katika maeneo machache.

Pwani ya kaskazini (Mikoa ya Tanga, Maeneo ya kaskazini mwa Morogoro, Pwani na Dar es Salaam pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba): Vipindi vya mvua zitakazoambatana na ngurumo za radi vinatarajiwa kwa baadhi ya maeneo.

Magharibi mwa nchi (Mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora): Mvua na ngurumo za radi vinatarajiwa katika baadhi ya maeneo.

Kanda ya kati (Mikoa ya Dodoma na Singida): Vipindi vya mvua zitakazoambatana na ngurumo za radi vinatarajiwa katika maeneo machache.

Nyanda za juu Kusini-magharibi (Mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa): Vipindi vya mvua zitakazoambatana na ngurumo za radi vinatarajiwa katika maeneo mengi.

Pwani ya kusini (Mikoa ya Mtwara na Lindi): Mvua na ngurumo vinatarajiwa katika maeneo mengi.

Kanda ya kusini (Mkoa wa Ruvuma na Maeneo ya kusini mwa Morogoro): Vipindi vya mvua zitakazoambatana na ngurumo za radi vinatarajiwa katika maeneo mengi.

Imetolewa na;

MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA