Machapisho
MATARAJIO YA HALI YA HEWA KWA TAREHE 21 - 31 MACHI, 2023
PakuaMWELEKEO WA MVUA KWA TAREHE 21-31 MACHI, 2023.
Kanda ya ziwa Viktoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Mwanza, Simiyu na Mara): Mvua na ngurumo za radi vinatarajiwa katika maeneo machache.
Nyanda za juu kaskazini-mashariki (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro): Mvua zinazoambatana na ngurumo za radi zinatarajiwa katika maeneo machache.
Pwani ya kaskazini (Mikoa ya Tanga, Maeneo ya kaskazini mwa Morogoro, Pwani na Dar es Salaam pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba): Mvua na ngurumo za radi vinatarajiwa.
Magharibi mwa nchi (Mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora): Mvua na ngurumo za radi vinatarajiwa kwa baadhi ya maeneo.
Kanda ya kati (Mikoa ya Dodoma na Singida): Mvua zinazoambatana na ngurumo za radi zinatarajiwa.
Nyanda za juu Kusini-magharibi (Mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa): Mvua na ngurumo za radi katika baadhi ya maeneo zinatarajiwa.
Pwani ya kusini (Mikoa ya Mtwara na Lindi): Mvua na ngurumo za radi vinatarajiwa katika baadhi ya maeneo.
Kanda ya kusini (Mkoa wa Ruvuma na Maeneo ya kusini mwa Morogoro): Mvua na ngurumo za radi vinatarajiwa katika baadhi ya maeneo.
Imetolewa na;
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA