Taarifa za Hali ya Hewa Kilimo
Jarida la Hali ya Hewa Tathmini ya Novemba 21-30, 2025 na Matazamio kwa Kipindi cha Disemba 1-10, 2025
PakuaJarida la hali ya Hewa Kilimo la msimu wa Novemba 2025 hadi Aprili_2026 (NDJFMA-Mvua za Msimu)
Pakua- Mvua za Chini ya Wastani hadi Wastani zinatarajiwa katika mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi, Singida na Dodoma na Wastani hadi Chini ya Wastani katika mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya, Songwe, Rukwa, Ruvuma, Mtwara na Lindi pamoja na kusini mwa mkoa wa Morogoro. Vipindi virefu vya ukavu na mtawanyiko wa mvua usioridhisha vinatarajiwa katika maeneo mengi.
- Mvua zinatarajiwa kuanza kati ya wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Oktoba, 2025 katika mikoa ya Tabora, Katavi na Kigoma; na kusambaa katika mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe pamoja na kusini mwa mkoa wa Morogoro kati ya wiki ya pili na ya tatu ya mwezi Novemba, 2025 na kuisha kati ya wiki ya nne ya mwezi Aprili na wiki ya kwanza ya mwezi Mei 2026 katika maeneo mengi. Kipindi cha nusu ya pili ya msimu (Februari-Aprili, 2026) kinatarajiwa kuwa na ongezeko la mvua ikilinganishwa na nusu ya kwanza (Novemba, 2025-Januari, 2026).
- Mvua za Chini ya Wastani zinazotarajiwa katika maeneo mengi zinaweza zikasababisha upungufu wa unyevu wa udongo na kuathiri ukuaji na maendeleo ya mazao na kupunguza mavuno hususani kwa mazao yanayotegemea mvua.
