Taarifa za Hali ya Hewa Kilimo
Jarida la Hali ya Hewa kilimo la Tathimini ya 01 - 10 Mei 2022 na Utabiri wa Mei 11 - 20, 2022
PakuaDONDOO ZA MEI 11 - 20, 2022
- Hali ya ukavu inayotarajiwa itasaidia shughuli za uvunaji na ukaushaji wa mazao.
- Wafugaji wanashauriwa kukusanya majani na chakula cha mifugo na kuvihifadhi vizuri kwa ajili ya matumizi ya baadae, pia kupata ushauri wa maafisa ugani juu ya utunzaji bora wa mifugo kwa kuzingatia hali ya hewa inayotarajiwa.
- Wakulima wanashauriwa kuendelea na shughuli za utunzaji wa mashamba na matumizi ya pembejeo kwa kufuata ushauri wa maafisa ugani.
Kwa taarifa zaidi tafadhali pakua ....
Jarida la Hali ya Hewa Kilimo la msimu wa mvua wa November 2021 hadi Aprili 2022
PakuaMUHTASARI
- Utabiri wa mvua za mwezi Novemba hadi Aprili (NDJFMA) ni mahususi kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka.
- Mvua zinatarajiwa kuwa za chini ya wastani hadi wastani katika maeneo mengi ya mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi, Singida, Dodoma, Rukwa, Songwe, Mbeya na Iringa na wastani hadi chini ya wastani katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Njombe, Ruvuma, Lindi, Mtwara na kusini mwa mkoa wa Morogoro.
- Vipindi virefu vya ukavu vinatarajiwa kati ya mwezi Novemba, 2021 na Januari, 2022.
- Mvua zinatarajiwa kuanza katika wiki ya tatu ya mwezi Novemba, 2021 katika maeneo mengi na kuisha katiya wiki ya pili na ya tatu ya mwezi Aprili, 2022.
- Malisho na maji ya mifugo vinatarajiwa kupungua hivyo kupelekea kongezeka kwa migororo ya wakulima nawafugaji.
Kwa taarifa zaidi tafadhali pakua...