Taarifa za Hali ya Hewa Kilimo
Jarida la Hali ya Hewa kilimo la Tathimini ya 01- 10 Machi 2023 na Utabiri wa Machi 11- 20, 2023
PakuaDONDOO ZA MARCH 11- 20, 2023
- Wakulima katika maeneo yanaopata mvua mara mbili kwa mwaka, wanashauriwa kuendelea na maandalizi ya mashamba kwa ajili ya msimu wa Masika. Hata hivyo wanashauriwa kupanda mazao yanayokoma haraka na kustahimili ukame.
- Kwa ujumla zao la mahindi katika maeneo yanayopata mvua za Msimu yapo katika hali ya kuridhisha.
- Wakulima, wafugaji na wavuvi wanahimizwa kuzingatia taarifa za hali ya hewa kwa shughuli na mipango kila siku
Kwa taarifa zaidi tafadhali pakua....
Jarida la Hali ya Hewa Kilimo la msimu wa mvua wa Machi hadi Mei 2023
PakuaMUHTASARI
- Mvua za wastani hadi chini ya wastani zinatarajiwa katika maeneo mengi ya nchi yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka isipokuwa maeneo machache ya mikoa ya Dar es salaam, Pwani (ikijumuisha Mafia), kaskazini mwa Morogoro pamoja na kisiwa cha Unguja ambapo mvua za wastani hadi juu ya wastani zinatarajiwa.
- Ongezeko la mvua linatarajiwa katika kipindi cha mwezi Mei 2023, hususan katika maeneo ya pwani ya kaskazini.
- Mvua za Masika zinatarajiwa kuanza mwezi Machi, katika maeneo mengi na zinatarajiwa kuisha katika wiki ya nne ya mwezi Mei 2023 katika maeneo mengi ingawa mwendelezo wa mvua za nje ya msimu unatarajiwa mwezi Juni 2023 katika maeneo machache ya ukanda wa pwani ya kaskazini.
- Mvua chache na zenye mtawanyiko usioridhisha katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za wastani hadi chini ya wastani zinaweza kusababisha upungufu wa unyevu kwenye udongo na upatikanaji wa maji kwa ajili ya shughuli za kilimo.
- Katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za wastani hadi juu ya wastani, unyevu wa udongo kupita kiasi unaweza kujitokeza na hivyo kuathiri ukuaji wa mazao ambayo hayahitaji maji mengi.
Kwa taarifa zaidi tafadhali pakua...