Taarifa za Hali ya Hewa Kilimo
Jarida la Hali ya Hewa kilimo la Tathimini ya 21 - 31 Julai 2022 na Utabiri wa Agosti 01 - 10, 2022
PakuaDONDOO ZA AGOSTI 01 - 10, 2022
- Kutokana na hali ya ukavu inayotarajiwa, wafugaji wanashauriwa kutumia maji na malisho kwa uangalifu.
- Mvua za nje ya msimu zinazotarajiwa hususan katika mikoa ya Pwani zinaweza kuathiri mikorosho iliyo katika hatua ya kutoa maua.
- Wakulima hususan wa maeneo yanayopata mvua mara mbili kwa mwaka wanashauriwa kuanza shughuli za kuandaa mashamba kwa ajiliya msimu mvua za Vuli.
Kwa taarifa zaidi tafadhali pakua
Jarida la Hali ya Hewa Kilimo la msimu wa mvua wa November 2021 hadi Aprili 2022
PakuaMUHTASARI
- Utabiri wa mvua za mwezi Novemba hadi Aprili (NDJFMA) ni mahususi kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka.
- Mvua zinatarajiwa kuwa za chini ya wastani hadi wastani katika maeneo mengi ya mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi, Singida, Dodoma, Rukwa, Songwe, Mbeya na Iringa na wastani hadi chini ya wastani katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Njombe, Ruvuma, Lindi, Mtwara na kusini mwa mkoa wa Morogoro.
- Vipindi virefu vya ukavu vinatarajiwa kati ya mwezi Novemba, 2021 na Januari, 2022.
- Mvua zinatarajiwa kuanza katika wiki ya tatu ya mwezi Novemba, 2021 katika maeneo mengi na kuisha katiya wiki ya pili na ya tatu ya mwezi Aprili, 2022.
- Malisho na maji ya mifugo vinatarajiwa kupungua hivyo kupelekea kongezeka kwa migororo ya wakulima nawafugaji.
Kwa taarifa zaidi tafadhali pakua...