Habari
Imewekwa:
Jun, 23 2025
TMA YASHIRIKI KATIKA MAONESHO YA KUADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2025.

Dodoma, tarehe 18 Juni 2025.
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imepata fursa ya kushiriki katika maonesho ya kuadhimisha wiki ya utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park, Dodoma kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2025.
Kupitia maonesho hayo wageni kutoka sekta mbalimbali nchini wameendelea kutembelea banda la TMA ikiwemo Waziri wa Nchi – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ili kujifunza masuala mbalimbali yalioandaliwa katika utoaji elimu juu ya huduma zitolewazo na TMA kwa manufaa ya jamii na maendeleo ya Taifa,
Kaulimbiu ya maonesho hayo ni “Kujenga Mifumo Thabiti ya Utoaji Huduma kwa Maendeleo Endelevu”.